Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, September 28

Jumapili, 28 Septemba 2014 20:05 Jaafari: Hakuna vikosi vya kigeni vya nchi kavu Iraq

Posted by mkachu  |  Tagged as: ,

Jaafari: Hakuna vikosi vya kigeni vya nchi kavu IraqIbrahim al Ja'afari Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq kwa mara nyingine ametahadharisha kuhusu tishio kuu la magaidi wa kitakfiri wa Daesh na kukanusha kuweko vikosi vya kigeni vya nchi kavu huko Iraq kwa ajili ya kukabiliana na kundi hilo la kigaidi. Mwanadiplomasia huyo wa ngazi ya juu wa Iraq amesisitiza kuwa serikali ya Baghdad haijawahi kuomba msaada wa vikosi vya nchi kavu kutoka nje kwa ajili ya kupambana na Daesh. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq ameyasema hayo pambizoni mwa mkutano wa 69 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani katika mazungumzo yake na Walid al Muallim Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria na mawaziri wenzake wa Uchina, Japan na Korea Kusini. Ibrahim Ja'aafari ametilia mkazo kwamba, msaada wa kutosha wa mashambulizi ya anga yanalisaidia jeshi la Iraq na vikosi vya kujitolea vya wananchi pamoja na wapiganaji wa Kikurdi wa Peshmerga kupambana na magaidi wa kitakfiri wa Daesh hivyo Iraq haihitajii vikosi vya kigeni vya nchi kavu katika kupambana na kundi hilo.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com