Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, September 28

Jumapili, 28 Septemba 2014 20:07 Wazayuni wawateka nyara vijana saba wa Kipalestina

Posted by mkachu  |  Tagged as: ,

Wazayuni wawateka nyara vijana saba wa Kipalestina
Askari wa Israel wamevamia nyumba kadhaa za Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu na kuwateka nyara vijana wasiopungua saba wa Kipalestina. Vijana hao wa Kipalestina wametekwa nyara baada ya wanajeshi wa Israel kuvamia nyumba zao katika miji ya Baytullahm, Quds, Husan na al Khalil mapema leo Jumapili. Wakazi wa maeneo hayo wamesema kuwa, vijana hao wamepelekwa kusikojulikana. Watano kati ya vijana hao wanadaiwa kuwalenga mawe wanajeshi wa utawala wa Kizayuni. Shirika la haki za binadamu la Palestina limesema kuwa, hivi sasa utawala wa Kizayuni unawashikilia Wapalestina 540 bila ya kuwafikisha mahakamani na kwamba kasi ya kutekwa nyara Wapalestina imeongezeka sana katika miaka ya hivi karibuni. Wazayuni wanaendelea kuwanyanyasa na kuwateka nyara kiholela Wapalestina huku hivi karibuni yaani tarehe 7 Julai utawala huo ukiwa umefanya mashambulizi ya kikatili dhidi ya Ukanda wa Ghaza na kuua mamia kwa mamia ya watu wasio na hatia kwa madai yasiyothibitishwa kuwa vijana watatu wa Kizayuni walitekwa nyara katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com