Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Saturday, March 28

Uchaguzi mkuu wafanyika leo nchini Nigeria

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Uchaguzi mkuu wafanyika leo nchini Nigeria
Wananchi waliotimiza masharti ya kupiga kura nchini Nigeria leo wameelekea kwenye vituo vya kupigia kura kwa lengo la kumchagua rais, wabunge na maseneta wa maeneo yao. Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Nigeria imetangaza kuwa, karibu watu milioni 68 na laki nane kutoka jumla ya watu milioni 173 wa nchi hiyo walijiandikisha kwenye daftari la kupiga kura nchini humo. Kwenye uchaguzi wa rais, kuna shakhsia 14 watakaochuana vikali kwenye uchaguzi huo ulioanza leo. Duru za habari zinasema, mchuano mkali utakuwa kati ya Rais Goodluck Jonathan kutoka chama tawala cha People's Democratic Party PDP na Jenerali mstaafu Muhammadu Buhari kutoka chama cha All Progressives Congress 'APC'. Rais Jonathan aliyeingia madarakani mwaka 2011, anahesabiwa kuwa rais wa kwanza kutoka kabila la Ijaw na pia ni kiongozi wa kwanza anayetoka eneo la kusini mwa Niger Delta. Buhari aliwahi kuiongoza Nigeria kuanzia mwaka 1983 hadi 1993 wakati nchi hiyo ilipokuwa ikitawaliwa na majenerali wa kijeshi. Buhari ameikosoa serikali ya Jonathan kwa kushindwa kulitokomeza kundi la kigaidi la Boko Haram pamoja na kuongezeka vitendo vya ufisadi wa kiserikali, umasikini na ukosefu wa ajira nchini humo. Taarifa zinasema kuwa, wasimamizi kutoka Umoja wa Afrika, Umoja wa Ulaya na Umoja wa Mataifa wako nchini Nigeria kwa lengo la kusimamia zoezi hilo

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com