Wizara ya Mwongozo na Wakfu ya Saudi Arabia imewataka mahatibu
misikitini kuyaungwa mkono makundi ya kigaidi. Taarifa iliyotolewa leo
na wizara hiyo imeeleza kuwa, makhatibu wa misikiti nchini humo
wametakiwa watoe hutuba zinazounga mkono makundi ya kigaidi na
yanayobeba silaha katika baadhi ya nchi za Kiislamu. Taarifa zinasema
kuwa, misimamo hiyo ya Saudi Arabia ni mwendelezo wa sera za utawala wa
Aal Saud za kuyaunga mkono makundi ya kitakfiri na kigaidi ambayo hadi
sasa yamesababisha ghasia na machafuko katika baadhi ya nchi za eneo la
Mashariki ya Kati zikiwemo Syria, Iraq, Lebanon na Yemen. Imeelezwa
kuwa, taasisi nyingi za kujitolea nchini Saudi Arabia ndizo
zinazodhamini misaada ya kifedha kwa makundi ya kigaidi na kitakfiri
yakiwemo Daesh, Jabhat Nusra na Taleban.
0 toamaon yako: