Leo ni Jumatatu tarehe 18 Mfunguo 3 Dhilhija mwaka 1435 Hijiria, inayosadifiana na tarehe 13 Oktoba mwaka 2014 Miladia.
Siku kama ya leo miaka 1425 iliyopita yaani tarehe 18 Mfunguo Tatu,
Mtume Muhammad (SAW) alimtangaza Imam Ali bin Abi Twalib (AS) kuwa
Khalifa na kiongozi wa Waislamu baada yake. Siku hiyo Bwana Mtume
alikuwa akirejea kutoka Makka alikokwenda kutekeleza ibada tukufu ya
hija na iliyokuwa hija yake ya mwisho. Mtume alisimama mahala palipoitwa
Ghadir Khum na baada ya kupanda sehemu yenye mwinuko aliuhutubia umma
mkubwa wa
Waislamu waliokuwa wamejumuika mahala hapo. Aidha Mtume (SAW)
aliinua mkono wa Imam Ali na kusema: "Yule ambaye mimi ninayatawala
mambo yake, huyu Ali ni Mwenye kuyatawala mambo yake pia, Ewe Mola!
Mfanye kipenzi Mwenye kumfanya Ali kipenzi, mfanye adui Mwenye kumfanyia
uadui na mnusuru mwenye kumnusuru." Ni kutokana na tukio hilo kubwa
katika historia ya Uislamu, ndipo siku hii ikajulikana kuwa sikukuu ya
Eidul Ghadir.
Siku kama ya leo miaka 2553 iliyopita mji wa kihistoria wa Babel
ulitekwa na Korush, mwasisi wa utawala wa kizazi cha Hakhamaneshi nchini
Iran. Ili kuweza kuudhibiti mji huo ambao ulikuwa na ngome kubwa na
imara, Korush alitoa amri ya kubadilishwa njia ya maji ya Mto Tigris
ambao ulikuwa ukipita ndani ya mji huo na kwa utaratibu huo askari wake
wakatumia njia ya maji ya mto huo kuingia na kisha kuuteka mji huo. Mji
huo ulioko kusini mwa eneo la Mesopotamia katika Iraq ya sasa ulikuwa
katika kilele cha maendeleo na nguvu kubwa katika kipindi hicho.
Na miaka 50 iliyopita bunge la kimaonyesho la Iran lilipasisha sheria
iliyowapa washauri wa kijeshi wa Marekani nchini kinga ya kutofikishwa
mahakamani iwapo wangepatikana na hatia ya aina yoyote. Kwa mujibu wa
sheria hiyo wahalifu wa Kimarekani wangehukumiwa nchini kwao kama
watatenda jinai nchini Iran, na mahakama za Iran hazikuwa na haki ya
kushughulikia kesi zao.
Sheria hiyo ilitambuliwa kuwa dharau kwa
taifa la Iran na iliyokiuka wazi kujitawala kwa nchi. Kwa msingi huo
hayati Imam Khomeini (MA) siku kadhaa baada ya kupasishwa sheria hiyo
bungeni alitoa hotuba ya kihistoria akieleza taathira zake na
kumshambulia vikali Mfalme Shah na Marekani. Baada ya hotuba hiyo Imam
Khomeini alikamatwa na kupelekwa uhamishoni
Monday, October 13
Jumatatu, Oktoba 13, 2014
Posted by mkachu |  Tagged as: leo katka hisory
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: