Waasi wa Sudan Kusini wameituhumu serikali ya nchi hiyo kuwa imetumia silaha za kemikali. Gabriel Tang, kamanda wa waasi katika jimbo la Upper Nile huko kaskazini mwa Sudan Kusini ameripoti kuwa mapigano kati ya wapinzani wenye silaha na jeshi la Sudan Kusini yameingia katika awamu mpya. Hii ni kwa sababu jeshi la Sudan Kusini limeanza kutumia silaha za kemikali dhidi ya wapinzani hao.
Tang amesema kuwa jeshi la Sudan Kusini lilitumia silaha za kemikali katika mapigano ya hivi karibuni katika miji ya Malakal na Ulang. Gabriel Tang ameongeza kuwa, siku mbili zilizopita jeshi la Sudan Kusini lilivurumisha makombora katika mji wa Malakal na kwamba wapiganaji wao kadhaa waliuawa baada ya kuvuta gesi ya sumu iliyokuwemo kwenye makombora hayo.
0 toamaon yako: