Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Monday, September 29

Onyo la China kuhusu Hong Kong

Posted by mkachu  |  Tagged as:

China yaonya mataifa ya kigeni kutoingilia maswala ya Hong Kong
Uchina imesema kuwa haitawavumilia wahaini kutoka nje ya nchi wanaounga mkono maandamano yasiyo halali nchini humo.
Kundi lijulikanalo kama Occupy Central ndilo linalolengwa kwa sababu limekuwa likiunga mkono juhudi za maandamano ya maelfu ya watu wanaounga mkono kuimraishwa kwa Demokrasia nchini Uchina.
Katika kile kinachoaminika kulenga maandamano yanayoendelea katika jimbo la Hong Kon, Uchina inaonya mataifa mengine yasijiingize kwa kila inachoamini na maswala ya ndani ya Uchina.
Uchina mara kwa mara hutoa onyo kwa mataifa mengine yasijiingize katika jimbo hilo lake linalotaka kuendesha mambo yake kivyake.

Serikali ya China inaamini kuwa Hong Kong Inauwezo wa kukabiliana na maandamano
Mapema mwezi huu Uchina iliudhika sana na matamshi ya Chris Patten, aliyekuwa wakati mmoja Gavana wa Hong Kong, aliposema kwamba Uingereza ina wajibu wa kutoa taarifa kwa niaba ya wakazi wa Hong Kong, eneo lililokuwa koloni yake wakati mmoja.
Baraza Kuu la Kitaifa la Uchina, ambalo ni kiungo muhimu katika Serikali, limesema kuwa lina imani kwamba Serikali ya Jimbo la Hong Kong, ina uwezo wa kukabiliana na maandamano hayo kibinafsi bila kuingiliwa na yeyote.
Kuna hofu kuu Hong Kong kuwa huenda Serikali Kuu ikatumia polisi wenye silaha kuzima maandamano hayo.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com