Makamu wa Rais wa Sudan amewataka wakazi wa eneo lililogubikwa na
ghasia na machafuko la Darfur kuwa macho na njama za maadui za kuzusha
mifarakano.
Ibrahim Ghandour amesema kuwa, maadui wa Sudan wanafanya
njama za kuibua mifarakano na hitilafu kati ya wakaazi wa eneo la Darfur
na kusisitiza kwamba, wakazi wa eneo hilo wanapaswa kuwa macho na
kuimarisha umoja na mshikamano wao kwa lengo la kuzima njama hizo za
maadui.
Makamu wa Rais wa Sudan amesema kuwa, chimbuko la ghasia na machafuko
katika eneo hilo ni uungaji mkono wa baadhi ya madola ya kigeni kwa
vibaraka wao na kusisitiza kwamba baadhi ya mashirika ya kijasusi ya
nchi za Magharibi yanafanya njama za kuzusha mapigano ya kikabila na
kikoo katika eneo hilo, ili yaweze kufikia malengo yao machafu. Makamu
wa Rais wa Sudan ameyataka makundi ya wanamgambo wanaobeba silaha katika
eneo hilo kuweka chini silaha zao na kuketi kwenye mazungumzo ya amani
na serikali ya Khartoum.
Eneo la Darfur lililoko magharibi mwa Sudan linajumuisha majimbo
matano na tokea mwaka 2003 hadi sasa linasumbuliwa na mapigano kati ya
makundi ya waasi na wanajeshi wa serikali.
Sunday, September 28
Browse: Home
» Habari za kitaifa na kimataifa
» Jumapili, 28 Septemba Ghandour: Wakazi wa Darfur wajiepushe na maadui
Jumapili, 28 Septemba Ghandour: Wakazi wa Darfur wajiepushe na maadui
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: