Sergei Lavrov Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Russia amesema kuwa, mazungumzo ya nyuklia kat i ya Iran na kundi la 5+1 takriban yameshafikia kwenye hatua ya makubaliano ya mwisho kwa asilimia 95, na kwamba hivi sasa yamesalia masuala mawili - matatu ambayo bado ni magumu na nyeti kati ya pande hizo mbili. Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Russia amesema kuwa, masuala hayo yanaweza kutatuliwa, iwapo litaangaliwa suala hilo kiutaalamu zaidi. Naye Muhammad Javad Zarif Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, mazungumzo yalikuwa jaddi na ya uwazi na kusisitiza kwamba pande mbili zimebakiwa na miezi miwili ya kutatua hitilafu zilizosalia. Dakta Zarif amesisitiza kuwa, masuala yaliyosalia siyo magumu sana, kwani yanaweza kutatuliwa iwapo litawekwa kando suala la utashi wa kisiasa. Duru ya saba ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran na kundi la 5+1 linalozijumuisha nchi za Uingereza, Ufaransa, Russia, China, Marekani na Ujerumani ilimalizika siku ya Ijumaa mjini New York, bila ya kutangazwa matokeo ya mazungumzo hayo. Vyombo visivyo rasmi vinaeleza kuwa, duru ijayo ya mazungumzo itafanyika mwezi ujao barani Ulaya na kwamba huenda makubaliano ya mwisho yakafikiwa tarehe 24 Novemba mwaka huu.
Sunday, September 28
Browse: Home
» Habari za kitaifa na kimataifa
» Jumapili, 28 Septemba 2014 Makubaliano ya Iran, 5+1 yamefikiwa kwa asilimia 95
Jumapili, 28 Septemba 2014 Makubaliano ya Iran, 5+1 yamefikiwa kwa asilimia 95
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: