Mkuu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi
ya Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, muundano dhidi ya
kundi la Daesh katika eneo la Mashariki ya Kati umeshindwa.
Ayatullah Hashemi Rafsanjani amesema hayo leo katika kongamano la kwanza la kitaifa lililobeba jina la Vyuo Vikuu na Suala la Kujihami Kutakatifu hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, mashambulizi ya anga ya muungano huo wa kimataifa dhidi ya maeneo ya Daesh hayawezi kulimaliza kundi hilo la kigaidi na ushahidi ni kwamba siku chache zilizopita kundi hilo lilishambulia eneo la Kobani la Syria katika mpaka wa nchi hiyo na Uturuki.
Ayatullah Rafsanjani aidha ameashiria namna Wamarekani wanavyokiri kuwa kama Iran haitausaidia muungano huo wa kimataifa dhidi ya kundi la kigaidi la Daesh, muungano huo hautoweza kulimaliza kundi hilo na kusisitiza kwamba: Marekani na waitifaki wake wameiwekea vikwazo Iran na huo ni moja ya uadui wao dhidi ya taifa la Iran, hivyo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haiwezi kuwa pamoja na Marekani na inafanya mambo yake kwa uhuru.
Ayatullah Hashemi Rafsanjani amesema hayo leo katika kongamano la kwanza la kitaifa lililobeba jina la Vyuo Vikuu na Suala la Kujihami Kutakatifu hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, mashambulizi ya anga ya muungano huo wa kimataifa dhidi ya maeneo ya Daesh hayawezi kulimaliza kundi hilo la kigaidi na ushahidi ni kwamba siku chache zilizopita kundi hilo lilishambulia eneo la Kobani la Syria katika mpaka wa nchi hiyo na Uturuki.
Ayatullah Rafsanjani aidha ameashiria namna Wamarekani wanavyokiri kuwa kama Iran haitausaidia muungano huo wa kimataifa dhidi ya kundi la kigaidi la Daesh, muungano huo hautoweza kulimaliza kundi hilo na kusisitiza kwamba: Marekani na waitifaki wake wameiwekea vikwazo Iran na huo ni moja ya uadui wao dhidi ya taifa la Iran, hivyo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haiwezi kuwa pamoja na Marekani na inafanya mambo yake kwa uhuru.
0 toamaon yako: