Kufuatia kuwekwa vikwazo vipya dhidi ya shakhsia kadhaa wa Venezuela na halikadhalika vitisho vya kiusalama vya
Rais Barack Obama dhidi ya nchi hiyo ya Amerika ya Latini, raia na serikali kadhaa za eneo hilo zimekosoa vikali siasa za rais huyo wa Marekani. Jamii ya nchi za Amerika ya Latini na zile za Bahari ya Caribbean kwa pamoja, zimepinga hatua na amri ya Rais Obama aliyeitaja Venezuela kuwa ni tishio la kiusalama dhidi ya Washington. Waziri wa Mambo ya Nje wa Ecuador Ricardo Patino ambaye nchi yake inashikilia uogozi wa Jumuiya ya nchi za Amerika ya Latini na visiwa vya Caribbean, ametangaza kuwa wanachama wote 33 wa jumuiya hiyo wanataka kuondolewa amri hiyo na badala yake kufanyike mazungumzo yatakayozingatia misingi ya kimataifa. Waziri wa Mambo ya Nje wa Ecuador ameongeza kuwa, mbali na wanachama wa jumuiya hiyo iliyotajwa, Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote kwa kifupi (NAM) siku ya Jumatano iliyopita, iliitaka pia Washington kubatilisha hukumu yake hiyo dhidi ya taifa la Venezuela. Kwa upande wake Rais Juan Evo Morales wa Bolivia ameelezea hatua ya Rais Barack Obama kuitaja Vinezuela kuwa tishio kwa nchi yake, kuwa ni kosa kubwa. Amesema kuwa hatua hiyo ni sawa na kuzitaja nchi zote za Amerika ya Latini kuwa tishio kwa maslahi ya Marekani na mfumo wake wa kibepari kutokana na nchi hizo kupinga kuporwa utajiri wao na Washington. Katika kikao cha mwisho cha nchi wanachama wa muungano wa ALBA kilichofanyika tarehe 18 mwezi Machi mwaka huu, washiriki walimtaka rais huyo wa Marekani kufutulia mbali amri hiyo iliyoitaja serikali ya Caracas kuwa tishio lisilo la kawaida kwa usalama wake. Ripoti hiyo ilieleza kuwa, Venezuela sio tishio kwa nchi yoyote na kinyume chake wananchi wake wameonyesha irada thabiti kwa ajili ya kuendeleza ushirikiano na mataifa mengine kieneo na kimataifa kwa ujumla. Muungano wa ALBA unaundwa na nchi za Amerika ya Latini ikiwemo Cuba, Venezuela, Bolivia, Ecuador, Nicaragua, Jamhuri ya Watu wa Dominican, Saint Vincent na Granadyn, St Lucia, Granada, Antigua na Barbara, St. Christopher na Saint Kitts na Nevis. Kabla ya hapo pia na katika kikao kilichofanyika mjini Quito, Ecuador muungano huo ulizitaka nchi wanachama wa mataifa ya Amerika ya Kusini unaofahamika kwa jina la Union de Naciones Suramericanas (UNASUR) kufanya juhudi za kuhakikisha vikwazo walivyowekewa shakhsia kadhaa wa Vinezuela vinaondolewa. Itakumbukwa kuwa tarehe Ttisa mwezi huu wa Machi, Rais Barack Obama alitoa amri ambayo iliitaja Venezuela kuwa tishio kwa usalama wake, amri ambayo iliambatana na kuyaweka katika orodha ya vikwazo, majina kadhaa ya viongozi wa nchi hiyo. Katika kujibu hatua hiyo, Caracas iliwaita maafisa wa ubalozi wake mjini Washington, huku Baraza la Kitaifa la Venezuela likimpa rais wa nchi hiyo uwezo maalumu kwa ajili ya kukabiliana na hujuma za ubeberu wa Marekani. Kufuatia amri hiyo wanaharakati wa asasi za kiraia nchini humo walianzisha kampeni iliyopewa jina la 'Venezuela sio Tishio' kampeni ambayo kwa muda wa siku nne tu zilizopita tayari imetiwa saini na watu milioni moja, katika kupinga siasa za rais wa Marekani dhidi ya taifa lao
IQRA FM RADIO
Saturday, March 28
Browse: Home
» Takwa la nchi za Amerika ya Latini la kuondolewa vitisho vya Marekani dhidi ya Venezuela
Takwa la nchi za Amerika ya Latini la kuondolewa vitisho vya Marekani dhidi ya Venezuela
Posted by mkachu | Tagged as:
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Sura ya Al Furqan, aya ya 41-44 (Darsa ya 628) Wasikilizaji wapenzi wa Darsa ya Qur'ani, Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: