Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Thursday, December 4

Rwasa aitahadharisha serikali Burundi na machafuko

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Rwasa aitahadharisha serikali Burundi na machafukoKiongozi wa chama cha upinzani cha FNL nchini Burundi ametahadharisha kuwa, taifa hilo linaweza kutumbukia kwenye ghasia na machafuko iwapo serikali haitowasikiza wadau katika siasa za nchi hiyo. Akizungumza kwenye mahojiano maalum na Idhaa hii, Agathon Rwasa amesema kuwa, mchakato wa kuandaa daftari la wapiga kura kupitia uandikishaji wa raia ni zoezi lililovurugika na ameitaka serikali kusitisha zoezi hilo mara moja. Rwasa amesema uchaguzi mkuu ujao unaweza kuwa nukta ya kuwaunganisha Warundi pamoja au kuwagawanya kwa kutegemea jinsi maandalizi yatakavyofanywa. Mkuu wa FNL amesema mustakabali wa siasa nchini Burundi unakumbwa na hatihati na kusisitiza kuwa serikali itabeba dhima iwapo machafuko yatatokea kutokana na upuuzaji wake wa hali ya mambo kwa hivi sasa.
Tayari muungano wa upinzani wa ADC-Ikibiri umejiondoa kwenye zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kufuatia dosari zilizojitokeza na kutishia kususia uchaguzi mkuu wa rais mwakani endapo serikali haitositisha zoezi hilo

Related Posts:

0 toamaon yako:

    Author

    CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

    uislam na maisha yake

    uzayuni

    swahili radio

    uislam na maisha

    mohamed waziri

    Subscribe to our Mailing List

    We'll never share your Email address.
    +255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com