Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, November 7

Upinzani Zimbabwe wataka wabunge 18 wafukuzwe

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Upinzani Zimbabwe wataka wabunge 18 wafukuzweChama cha Upinzani cha Zimbabwe cha Movement for Democratic Change (MDC) kimetaka kuwafukuza bungeni wawakilishi 18 ambao si wabunge tena wa chama hicho. Wabunge hao ni pamoja na Tendai Biti katibu mkuu wa zamani wa MDC na waziri wa fedha ambaye amefukuzwa  chamani na mkuu wa chama hicho Morgan Tsvangirai. Chama hicho kimeliambia bunge kuwa wawakilishi hao 18 ambao walichaguliwa kama wabunge wa MDC hawakiwakilishi tena chama hicho. Biti na wenzake walikuwa wakijaribu kumuuzulu Tsvangirai chamani kwa kushindwa kumuangusha Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe katika uchaguzi wa rais.
Mpasuko huo umekidhoofisha chama hicho cha upinzani kinachompinga Mugabe ambaye yupo madarakani tangu nchi hiyo ilipojipatia uhuru mwaka 1980.
 Wiki iliyopita Tsvangirai alichaguliwa tena bila kupingwa kukiongoza chama cha MDC.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com