Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Monday, October 20

Jumapili 24 Dhulhijjah 1435

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Leo ni Jumapili tarehe 24 Mfungo Tatu Dhulhijjah mwaka 1435 Hijria, inayosadifiana na tarehe 19 Oktoba 2014 Miladia.
Jumapili 24 Dhulhijjah 1435Siku kama ya leo miaka 1426 iliyopita kwa mujibu wa riwaya mashuhuri Mtume Muhammad (saw) akiwa pamoja na binti yake Bibi Fatima (as), mkwewe Ali bin Abi Twalib (as) na wajukuu wake wawili Hassan na Hussain (as) aliondoka mjini Madina kwenda kufanya mdahalo na maapizano na viongozi wa Wakristo wa eneo la Najran juu ya dini ya kweli. Tukio hilo linaelezwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu katika aya za 60 na 61 za sura ya Aal Imran. Wakati viongozi wa Najran walipoona Mtume amekuja katika mdahalo huo akiwa na watu wanne tu wa Nyumba yake tukufu walipigwa na mshangao na kuelewa kwamba, dua ya laana ya mtukufu huyo kwa mtu ambaye angesema uongo ingekubaliwa. Katika hali hiyo askofu wa Najran alisema: "Ninaziona nyuso ambazo iwapo zitamuomba Mwenyezi Mungu aung'oe mlima mkubwa zaidi mahala pake basi dua yao itajibiwa papo hapo. Hivyo haitakuwa sahihi kufanya mdahalo na watu hawa watakatifu kwani yumkini kizazi chetu chote kikaangamia." Baada ya hapo askofu huyo wa Najran alimuomba msamaha Mtume (saw). Tukio hilo la kihistoria lilidhihirisha haki na ukweli wa dini tukufu ya Kiislamu na utukufu na nafasi aali ya Ahlulbait wa Mtume Muhammad (saw).
Siku kama ya leo miaka 38 iliyopita, Ali Hassan Salameh mmoja kati ya viongozi wa juu wa Harakati ya Ukombozi wa Palestina PLO aliuawa shahidi nchini Lebanon kupitia njama za vibaraka wa Shirika la Ujasusi la utawala haramu wa Israel MOSSAD. Salameh alikuwa afisa wa usalama wa PLO na aliuawa shahidi baada ya kuripuka bomu lililotegwa katika gari lake mjini Beirut. Jinai hiyo ya utawala haramu wa Kizayuni ndani ya Lebanon kwa mara nyingine iliweka wazi ugaidi na uvamizi wa Israel dhidi ya ardhi ya nchi nyingine.
Siku kama ya leo miaka 11 iliyopita, alifariki dunia Ali Ezzat Begovic, mwanasiasa na mwandishi wa Bosnia Herzegovina. Ali Begovic alizaliwa mwaka 1925 na kupata taaluma ya sheria katika Chuo Kikuu cha Sarajevo katikati mwa Bosnia. Alianza kupambana na utawala wa kikomunisti wa Yugoslavia ya zamani akiwa kijana mdogo na kufungwa jela mara kadhaa. Mwaka 1989 Ali Begovic aliasisi chama kipya cha siasa kwa jina la Democratic Action kilichokuwa na nafasi kubwa katika uhuru wa Bosnia mwaka 1991. Mwanasiasa huyo wa Kiislamu ambaye baada ya uhuru wa taifa hilo alichaguliwa kuwa rais, alikuwa na nafasi kubwa katika kuwatetea raia wa Bosnia, katika mashambulizi ya askari wa Serbia na dhidi ya Waislamu wa nchi hiyo.
Na siku kama ya leo miaka 70 iliyopita, vita kati ya vikosi vya Japan na jeshi la Marekani vilianza katika visiwa vya Ufilipino. Itakumbukwa kuwa, wakati wa kuanza Vita Vikuu vya Pili vya Dunia, Ufilipino ilishambuliwa na Japan na kwa muda mfupi ikawa imedhibitiwa na kukaliwa kwa mabavu. Hata hivyo baada ya kushindwa Ujerumani ya Kinazi katika Vita vya Pili vya Dunia, majeshi ya Marekani chini ya usimamizi wa Douglas MacArthur yaliishambulia Ufilipino na kuyatoa majeshi ya Japan katika ardhi ya nchi hiyo na kisha kuanzisha kambi za kijeshi nchini humo.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com