Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Monday, October 20

Jumanne, Oktoba 14, 2014

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Leo ni Jumanne tarehe 19 Dhilhaji 1435 Hijria sawa na 14 Oktoba 2014.
Jumanne, Oktoba 14, 2014Siku kama ya leo miaka 15 iliyopita alifariki dunia kiongozi wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Nyerere alizaliwa Butiama mkoani Mara mwaka 1922. Mwaka 1955 aliingia katika ulingo wa siasa huku akiongoza chama cha Tanganyika African National Union (TANU). Mwaka 1961 Nyerere alikuwa Waziri Mkuu wa Tanganyika na mwaka mmoja baadaye akawa rais wa nchi hiyo. Kutokana na juhudi zake mwaka 1964 ziliungana Tanganyika na Zanzibar na kuunda nchi moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nyerere aliendelea kuongoza nchi hiyo hadi mwaka 1985 ambapo aliachia hatamu za uongozi. Hata hivyo Nyerere aliendelea kuwa na ushawishi mkubwa katika siasa za Tanzania hadi alipofariki dunia.
Siku kama ya leo miaka 61 iliyopita Wazayuni wa Israel walivamia kijiji cha Qibya kilichoko katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan huko Palestina na kufanya jinai kubwa za kutisha. Katika mashambulizi na uvamizi ulioendelea katika kijiji hicho kwa muda wa siku mbili, Wazayuni walifanya mauaji na ukatili mkubwa dhidi ya raia wa Kipalestina wasio na hatia. Mbali na Wazayuni hao kuwaua na kuwajeruhi kwa umati raia zaidi ya 42 wa Kipalestina, askari wa Israel waliokuwa wakiongozwa na waziri mkuu wa zamani wa utawala huo wa kigaidi Ariel Sharon walibomoa makumi ya nyumba na shule za kijiji hicho. Mauaji hayo ya halaiki ni miongoni mwa mifano ya ugaidi wa utawala ghasibu wa Israel hususan waziri mkuu wa zamani wa utawala huo Ariel Sharon.
Na tarehe 19 Dhulhija mwaka 1257 Hijria alizaliwa Ayatullah Sayyid Muhammad Tabatabai, mmoja wa wasomi wakubwa wa Kiislamu na wapigania uhuru wa Iran. Wakati wa mapinduzi ya kikatiba nchini Iran, Sayyid Muhammad Tabatabai alikuwa akihesabika kuwa miongoni mwa viongozi wakubwa wa mapinduzi hayo. Tabatabai alishirikiana na Sayyid Abdullah Behbahani ambaye naye alikuwa mmoja wa viongozi wa harakati ya kikatiba dhidi ya utawala wa Qajari nchini Iran.
Mbali na kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, Sayyid Tabatabai alikuwa mwanazuoni hodari na alifanya bidii kubwa kueneza mafundisho ya Kiislamu

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com