Leo ni Ijumaa tarehe 15 Mfunguo Tatu Dhilhaji 1435 Hijria sawa na tarehe 10 Oktoba 2014 Milaadia.
Siku
kama ya leo miaka 1221 iliyopita kulingana na kalenda ya Hijria,
alizaliwa Imam Ali Naqi (AS) mashuhuri kwa lakabu ya al-Hadi, mmoja wa
wajukuu wa Mtume Muhammad SAW, katika mji mtakatifu wa Madina. Baada ya
kuuawa shahidi baba yake, yaani Imam Jawad AS, Imam Hadi alichukua
jukumu zito la Uimamu na kuongoza Umma wa Kiislamu. Zama za Uimamu wake
zilisadifiana na kipindi cha utawala wa ukoo wa Bani Abbas, na
Mutawakkil ndiye aliyekuwa ameshika hatamu za uongozi wakati huo. Baada
ya mtawala huyo kuhisi kuwa Imam Hadi (as) na wafuasi wake walikuwa
hatari kwa utawala wake, aliamrisha Imam atolewe Madina na kuhamishiwa
Samarra, Iraq ili amuweke chini ya uangalizi. Licha ya hayo yote, lakini
Imam Naqi aliendelea kueneza mafunzo sahihi ya dini tukufu ya Kiislamu.
Miaka
283 iliyopita katika siku kama hii ya leo mnamo mwaka 1731, alizaliwa
huko katika mji wa Nice, Henry Cavendish, mwanafalsafa na tabibu wa
Kiingereza. Cavendish alikuwa mwalimu wa masomo ya fikizikia, kemia na
udaktari. Henry Cavendish alikuwa mtu wa kwanza aliyethibitisha kuwa
gesi ya hyadrogen ni nyepesi zaidi kuliko hewa ya kawaida. Cavendish
aliaga dunia m
waka 1810.
Na miaka 112 iliyopita katika siku kama ya
leo, kilifanyika kikao cha kwanza cha Mahakama ya Kimataifa ya
Upatanishi ya Hague huko Uholanzi. Mahakama ya Upatanishi ya Hague
iliundwa mwaka 1899 kufuatia pendekezo la Tezar Nicolaus wa Pili, Mfalme
wa Urusi ya zamani. Mahakama hiyo ni moja kati ya taasisi za kisheria
za kimataifa na iko chini ya Umoja wa Mataifa. Mahakama hiyo ina majaji
15 ambao huchaguliwa na Baraza Kuu na Baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa bila ya kutilia maanani utaifa wao.
Miongoni mwa majukumu ya
Mahakama ya Upatanishi ya Kimataifa ya Hague, Uholanzi ni kutatua
hitilafu kati ya nchi mbalimbali na kuzuia vita kati ya nchi hizo.
IQRA FM RADIO
Sunday, October 12
Ijumaa, Oktoba 10, 2014
Posted by mkachu |  Tagged as: leo katka hisory
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

Facebook
Twitter
RSS
0 toamaon yako: