Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Monday, September 29

Jumatatu, 29 Septemba 2014 Uingereza yaondoa tahadhari kuhusu Kenya

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Serikali imeondoa tahadhari iliyowekea raiya wake kuingia Kenya 
 

Uingereza imeondoa tahadhari iliyokuwea imetoa kwa raia wake dhidi ya Kusafiri Kenya.
Tahadhari hiyo kwa ukubwa likuwa inalenga maeneo ya mitaa ya mabanda, na baadhi ya maeneo ya Pwani ambako ilihofiwa kuwa raia wa kigeni wanalengwa kwa mashambulio ya kigaidi.
Hatua hiyo ya kuondolewa tahadhari kwa raia wa Uingereza kusafiri Kenya, inaanza kutekelezwa mara moja.
Tahadhari hiyo ilikuwa imewekwa baada ya machafuko yaliyotokea nchini Kenya baada ya uchaguzi mkuu yapata miaka saba iliyopita.
Wizara ya mambo ya nje ya Uingereza imewasiliana na wizara ya ndani ya nchi hiyo kwamba hali ya hatari imeshuka kwa kiasi kikubwa.
Wizara hizo zimesema kuwa tahadhari kama hizo hutolewa kuambatana na sera za nchi hiyo za kuwatolea usalama raia wake kote duniani licha ya taifa linalozungumziwa.
Serikali ya Kenya ilikuwa imelalamika kuwa tahadhari kama hizi zinazotolewa na mataifa ya Magharibi hazina msingi na zinaathiri uchumi wa nchi hiyo.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com