Leo ni Jumatano tarehe 28 Dhulqaada 1435 Hijria sawa na 24 Septemba 2014.
Miaka 36 iliyopita katika siku kama hii ya leo, vikosi vya usalama vya utawala wa Baath wa Iraq vikishirikiana na utawala wa Shah viliizingira nyumba ya Imam Khomeini Mwenyezi Mungu amrehemu, mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu huko Najaf. Kwa kuzingatia uhusiano mzuri uliokuwa nao na utawala wa Shah, utawala wa zamani wa Iraq ulimtaka Imam Khomeini asifanye mahojiano na waandishi wa habari, kutoa taarifa, kuhutubia wala kuzungumzia hali ya mambo ya Iran dhidi ya utawala wa Shah. Imam Khomeini aliwajibu kwa kusema kuwa: "Natatekeleza wajibu wangu wa kisheria popote pale nitakapokuwa." Baada ya hapo, serikali ya wakati huo ya Iraq, ikamlazimisha Imam Khomein kuondoka Iraq na hatua hiyo ikaandaa uwanja wa hijra ya kihistoria ya Imam Khomeini ya kuelekea Paris, Ufaransa na kupamba moto utangulizi wa ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Siku kama ya leo miaka 40 iliyopita, Guinea Bissau ilitangaza uhuru wake kutoka kwa mkoloni Mreno. Guinea Bissau iligunduliwa mwaka 1446 na Mwana Mfalme Henry aliyekuwa akitawala Ureno pamoja na wenzake na kuwa koloni la nchi hiyo. Guinea Bissau ambayo ilikuwa ikijulikana kwa jina la Guinea Ureno, ilikuwa miongoni mwa vituo vya biashara ya utumwa ya wazungu katika karne za 17 na 18. Na hatimaye ilipofika mwaka 1974, Ureno ikakubali kuwa huru nchi ya Guinea Bissau. Guinea Bissau iko kaskazini magharibi mwa Afrika na katika pwani ya bahari ya Atlantic.
Na tarehe 28 Dhilqaada miaka 1075 iliyopita mwanazuoni wa Kiislamu Abul Qasim Tabarani, alifariki dunia katika mji wa kihistoria wa Isfahan nchini Iran. Tabarani alikuwa miongoni mwa wanazuoni mashuhuri wa hadithi wa karne ya nne Hijria na alifanya safari katika nchi nyingi za Kiislamu kwa ajili ya kukusanya hadithi za Mtume (saw). Alianza kufundisha na kulea wanafunzi wengi baada ya utafiti na uchunguzi wa miaka 33.
Tabarani ameandika vitabu vikubwa vitatu vya hadithi kwa majina ya Al Muujamul Kabiir", al Muujamul Wasiit na al Muujamus Swaghir.
Alkhamisi, 26 Septemba, 2014
Leo ni Alkhamisi tarehe 20 Dhilqaada 1434 Hijria sawa na tarehe 26 Septemba 2013.
Miaka 51 iliyopita katika siku kama ya leo mfumo wa kisultani huko Yemen ya Kaskazini ambao viongozi wake walikuwa wakijiita Imam, ulibatilishwa. Katika siku hiyo Kanali Abdallah Salal alifanya mapinduzi ya kijeshi na kuhitimisha mfumo wa Kisultani na kuasisi mfumo wa jamhuri nchini humo. Baada ya mapinduzi hayo Muhammad Badr aliyekuwa mfalme wa mwisho wa Yemen alianzisha vita dhidi ya utawala mpya wa nchi hiyo kwa uungaji mkono wa Saudi Arabia. Katika upande mwingine Rais Gamal Abdel Nasser wa Misri alituma wanajeshi wa nchi hiyo huko Yemen ili kumsaidia Abdallah Salal katika vita hivyo. Hata hivyo baada ya kupita miaka minne ya vita, pande husika katika vita hivyo zilifikia mapatano na wafuasi wa Imam Badr wakatupilia mbali madai yao ya awali.
Miaka 106 iliyopita katika siku kama ya leo New Zealand inayopatikana mashariki mwa Australia ilipata uhuru. Mwaka 1769 kisiwa cha New Zealand kilikuwa koloni la Uingereza. New Zealand ilizidi kukoloniwa katika karne ya 19 sambamba na kuingia nchini humo wahamiaji wengi wa Kiingereza.
Na siku kama ya leo miaka 125 iliyopita Thomas Stearns Eliot maarufu kwa jina la T.S Eliot, mwanafasihi na mshairi maarufu wa Kiingereza alizaliwa. Mwaka 1922 Eliot alipata umashuhuri kwa kuchapisha diwani ya mashairi aliyoipa jina la "Ardhi Iliyoharibiwa". Mshairi huyo ameandika vitabu vingi vinavyoakisi hisi yake ya kushikamana na kufuata mafundisho ya dini.
Miongoni mwa vitabu vya Thomas Stearns Eliot ni 'Vita Visivyokuwa na Maana', 'Msitu Mtakatifu' na 'Jinai Kanisani
Miaka 51 iliyopita katika siku kama ya leo mfumo wa kisultani huko Yemen ya Kaskazini ambao viongozi wake walikuwa wakijiita Imam, ulibatilishwa. Katika siku hiyo Kanali Abdallah Salal alifanya mapinduzi ya kijeshi na kuhitimisha mfumo wa Kisultani na kuasisi mfumo wa jamhuri nchini humo. Baada ya mapinduzi hayo Muhammad Badr aliyekuwa mfalme wa mwisho wa Yemen alianzisha vita dhidi ya utawala mpya wa nchi hiyo kwa uungaji mkono wa Saudi Arabia. Katika upande mwingine Rais Gamal Abdel Nasser wa Misri alituma wanajeshi wa nchi hiyo huko Yemen ili kumsaidia Abdallah Salal katika vita hivyo. Hata hivyo baada ya kupita miaka minne ya vita, pande husika katika vita hivyo zilifikia mapatano na wafuasi wa Imam Badr wakatupilia mbali madai yao ya awali.
Miaka 106 iliyopita katika siku kama ya leo New Zealand inayopatikana mashariki mwa Australia ilipata uhuru. Mwaka 1769 kisiwa cha New Zealand kilikuwa koloni la Uingereza. New Zealand ilizidi kukoloniwa katika karne ya 19 sambamba na kuingia nchini humo wahamiaji wengi wa Kiingereza.
Na siku kama ya leo miaka 125 iliyopita Thomas Stearns Eliot maarufu kwa jina la T.S Eliot, mwanafasihi na mshairi maarufu wa Kiingereza alizaliwa. Mwaka 1922 Eliot alipata umashuhuri kwa kuchapisha diwani ya mashairi aliyoipa jina la "Ardhi Iliyoharibiwa". Mshairi huyo ameandika vitabu vingi vinavyoakisi hisi yake ya kushikamana na kufuata mafundisho ya dini.
Miongoni mwa vitabu vya Thomas Stearns Eliot ni 'Vita Visivyokuwa na Maana', 'Msitu Mtakatifu' na 'Jinai Kanisani
0 toamaon yako: