Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, September 26

Jumamosi, 27 Septemba 2014 08:34 Wimbi la kutiwa mbaroni wanachama wa Ikhwanul Muslimin nchini Misri

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Wimbi la kutiwa mbaroni wanachama wa Ikhwanul Muslimin nchini Misri
Serikali ya Misri inaendelea kutumia mabavu dhidi ya wanachama wa Ikhwanul Muslimin. Hatua ya hivi karibuni kabisa iliyochukuliwa na serikali ya Misri ni ile ya kuwahukumu kifungo cha maisha jela, wanachama 73 wa kundi hilo. Maafisa wa mahakama wa nchi hiyo wamedai kuwa, wanachama hao wamepatikana na hatia ya kufanya vitendo vya uharibifu na uvunjifu wa amani. Abdullah Barakat, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kiislamu ambaye pia ni miongoni mwa wanachama waandamizi wa Ikhwanul Muslimin nchini Misri naye amekumbwa na tuhuma hizo hizo na amehukumiwa kifungo cha maisha jela na kulipa fidia ya dola 2,769. Hivi karibuni pia kulisambazwa habari za kutiwa mbaroni wanachama 123 wa Ikhwanul Muslimin katika mikoa 13 ya Misri. Inavyoonekana ni kuwa watawala wa Misri wanatumia mahakama ili kuwabana zaidi na zaidi kisiasa na kijamii wanachama wa Ikhwanul Muslimin. Hivi sasa viongozi wa daraja la kwanza, wa daraja la pili na wa daraja la tatu wa kundi hilo, wote wako jela wakiongozwa na Muhammad Morsi, Rais aliyechaguliwa na wananchi na kupinduliwa na jeshi. Muhammad Badie, kiongozi mwingine mkubwa wa Ikhwanul Muslimin naye ni miongoni mwa wanachama wa kundi hilo aliyehukumiwa kifungo cha maisha jela. Itakumbukwa kuwa, wakati wa kampeni za kuwania urais nchini Misri, Rais Abdul Fattah Sisi aliahidi kuwa akichaguliwa kuwa Rais wa nchi hiyo ataiangamiza kikamilifu Ikhwanul Muslimin nchini humo, na atahakikisha wanachama wote wa harakati hiyo wanafutwa nchini Misri. Baada ya kutoa matamshi hayo, wimbi la kuwatia mbaroni wanachama wa kundi hilo lilianza. Baadhi ya duru za habari zimetangaza kuwa, zaidi ya wanachama 1,400 wa Ikhwanul Muslimin wameshatiwa nguvuni hadi hivi sasa huko Misri. Kosa kubwa la wanachama hao ni kushiriki katika maandamano ya amani. Hata hivyo serikali ya Cairo inawabandika tuhuma za kuhatarisha usalama wa taifa na kutoa adhabu kali dhidi yao ambapo wengi wao wamehukumiwa kifo au kifungo cha maisha jela, adhabu ambazo zimelalamikiwa sana duniani. Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa imeelezea kusikitishwa sana na adhabu zinazotolewa na serikali ya Misri dhidi ya wanachama wa Ikhwanul Muslimin na kutaka wahukumiwe kiuadilifu. Shirika la Haki za Binadamu la Kiarabu lenye makao yake nchini Uingereza nalo limetoa tamko likisema kuwa adhabu hiyo ni uvunjaji wa wazi wa sheria za ndani ya Misri na za kimataifa. Shirika hilo limezitaka taasisi za kimataifa ukiwemo Umoja wa Afrika AU kuchukua hatua za haraka za kuwaokoa wanachama hao wa Ikhwanul Muslimin. Waziri wa Mambo ya Nje wa Sweden naye amekosoa adhabu zilizotolewa dhidi ya wanachama wa kundi hilo huko Misri na kuitaka jamii ya kimataifa iingilie kati. Wakati huo huo harakati ya Ikhwanul Muslimin ya Misri nayo imetoa tamko mjini London Uingereza na kuzitaja adhabu kali zinazotolewa dhidi ya wanachama wa kundi hilo na wapinzani wengine nchini Misri kuwa ni za kutisha na kusema kuwa harakati hiyo itatumia njia zote za amani kuhakikisha inawag'oa madarakani majenerali wa kijeshi nchini Misri.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com