Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, November 21

Mahmoud Abbas ataka kusitishwa jinai za Israel

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Mahmoud Abbas ataka kusitishwa jinai za IsraelRais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amewaandikia barua shakhsia kadhaa wa kisiasa ulimwenguni akitaka kuweko uingiliaji kati wa haraka ili kukomeshwa hujuma na jinai za utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Wapalestina huko Quds inayokaliwa kwa mabavu.
Katika barua yake kwa Bani Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, John Kerry Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani, Sergey Lavrov Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia, Federica Mogherini Mkuu mpya wa Siasa za Kigeni wa Umoja wa Ulaya na Tony Blair Mjumbe wa Kamati ya Pande Nne ya Amani ya Mashariki ya Kati, Rais Mahmoud Abbas amewataka shakhsia hao kuulazimisha utawala wa Kizayuni wa Israel uhitimishe jinai zake dhidi ya wananchi wa Palestina. Aidha Mahmoud Abbas amewataka shakhsia hao kuiunga mkono azma ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina ya kutambuliwa nchi ya Palestina kwa mujibu wa mipaka ya mwaka 1967 mji mkuu wake ukiwa Baytul Muqaddas. Hayo yanajiri katika hali ambayo, katika siku za hivi karibuni utawala wa Kizayuni wa Israel umeshadidisha hujuma na mashambulio yake dhidi ya Wapalestina na katika msikiti wa al-Aqswa huko Baytul Muqaddas.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com