Leo ni Jumanne tarehe 12 Dhilhaji 1435 Hijria sawa na Oktoba 7, 2014.
Miaka 65 iliyopita, Ujerumani
ya Mashariki iliasisiwa na kuwa na mfumo wa Jamhuri ya Kidemokrasia.
Katika miezi ya mwishoni mwa Vita vya Pili vya Dunia, Shirikisho la
Umoja wa Sovieti liivamia na kuikalia kwa mabavu ardhi ya Ujerumani ya
Mashariki, na madola ya Magharibi yakadhibiti sehemu ya magharibi mwa
nchi hiyo. Hata hivyo baadaye Umoja wa Sovieti ulijitoa katika Baraza la
Makamanda wa Waitifaki baada ya kutofautiana na madola ya Magharibi juu
ya namna ya kuiendesha nchi hiyo.
Na siku kama ya leo miaka 74
iliyopita, yaani tarehe saba Oktoba mwaka 1940 majeshi ya Ujerumani ya
Kinazi yaliidhibiti na kuikalia kwa mabavu ardhi ya Romania katika
kipindi cha Vita Vikuu vya Pili vya Dunia. Kwa utaratibu huo, uwanja wa
majeshi ya Ujerumani wa kuishambulia ardhi ya lililokuwa Shirikisho la
Umoja wa Sovieti mnamo Juni 1941 ukawa umeandaliwa.
Facebook
Twitter
RSS
0 toamaon yako: