Leo ni Jumapili tarehe tatu Dhul-Hijja mwaka 1435 Hijria, inayosadifiana na tarehe 28 Septemba 2014 Miladia.
Siku kama ya leo miaka 1073 iliyopita alizaliwa huko katika mji wa
Birun karibu na Khorazm, moja kati ya miji ya zamani ya Iran Abu Raihan
Biruni msomi, mnajimu na mwanahisabati mkubwa wa Kiirani. Abu Raihan
Biruni alikuwa mtaalamu katika elimu za historia, jiografia unajimu na
hisabati. Akiwa safarini nchini India, msomi huyo wa Kiirani alikutana
na kufanya mazungumzo na maulamaa na watawala wa za
ma hizo na baada ya
kujifunza lugha ya Sanskrit ambayo ni lugha ya kale ya Kihindi Abu
Raihan alikusanya taarifa muhimu alizokuwa akizihitaji kwa ajili ya
kuandika kitabu chake alichokiita 'Tahqiq Ma Lilhind'. Mbali na kitabu
hicho msomi huyo alipata kuandika vitabu vingi katika nyanja tofauti
zikiwemo za unajimu na mantiki.
Siku kama ya leo miaka 123 iliyopita alifariki dunia mwandishi
mashuhuri wa Kimarekani Herman Melville. Melville alizaliwa mwaka 1819
na kuanza kujishughulisha na ubaharia. Katika moja ya safari zake, meli
ya Melville ilizama na kusukumwa na maji hadi katika kisiwa kimoja
ambako wakazi wake walikuwa wakila watu. Melville ameelezea kisa hicho
na jinsi alivyowatoroka watu hao katika kitabu alichokipa jina la Typee.
Kuchapishwa kitabu hicho, kuliongeza zaidi umashuhuri wake.
Siku kama ya leo miaka 44 iliyopita, alifariki dunia rais wa
zamani wa Misri Gamal Abdel Nasser. Abdel Nasser alizaliwa mwaka 1916
Miladia. Aidha alishiriki katika vita vya kwanza vya Waarabu na utawala
wa Kizayuni hapo mwaka 1948 na kufanya mapinduzi ya kijeshi kwa
kushirikiana na Jenerali Najib, dhidi ya Mfalme Faruq 1952 na kuung'oa
utawala wa kisultani nchini humo. Miaka miwili baadaye Gamal Abdel
Nasser alimuondoa madarakani mshirika wake Jenerali Najib na kuchukua
jukumu la kuiongoza Misri sanjari na kufanya juhudi za marekebisho,
kupambana na ukoloni na utawala ghasibu wa Israel. Mwaka 1956
aliutaifisha mfereji wa Suez na kuufanya kuwa mali ya Misri, hatua
iliyozifanya nchi za Ufaransa, Uingereza na utawala wa Kizayuni
kuishambulia Misri. Hatua ya viongozi wa Misri ya kujibu hujuma hiyo,
iliongeza umaarufu wa Abdel Nasser nchini Misri na ulimwenguni kwa
ujumla.
Siku kama ya leo miaka 18 iliyopita, Baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa lilitoa azimio likiutaka utawala wa Kizayuni kukomesha
operesheni ya kuchimba mashimo chini ya msikiti wa al Aqsa huko
Palestina inayokaliwa kwa mabavu. Rasimu ya azimio hilo ililaani
uchimbaji huo wa mashimo kinyume cha sheria chini ya eneo hilo takatifu.
Hata hivyo upinzani wa Marekani ulipelekea kuondolewa kipengee hicho
katika azimio hilo.
Uchimbaji huo wa mashimo chini ya Msikiti wa al
Aqsa na utawala huo ghasibu, ulizusha machafuko ya umwagaji damu mkubwa
hapo tarehe 23 Septemba 1996 kati ya askari wa Israel na Wapalestina
ambapo askari hao waliua na kujeruhi mamia ya Wapalestina.
Na siku kama ya leo miaka 14 iliyopita Intifadha ya wananchi wa
Palestina kwa mara nyingine tena ilipamba moto. Hatua ya Ariel Sharon
kiongozi wa chama chenye misimamo mikali cha Likud na mhusika mkuu wa
mauaji ya halaiki ya Wapalestina katika kambi za Sabra na Shatila ya
kuingia katika Msikiti wa al Aqswa na kuuvunjia heshima msikiti huo
mtukufu, iliwatia hasira Wapalestina na kuwafanya waanzishe maandamano
na mapambano makubwa dhidi ya utawala huo wa Israel.
Sunday, September 28
Jumapili, Septemba, 28, 2014
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa, leo katka hisory
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: