Hali tete inatawala katika jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania
kutokana na mvua ya masika iliyonyesha kwa siku tatu na kusababisha vifo
vya watu watano, huku nyumba nyingi zikiwa zimezingirwa na maji. Maeneo
yaliyoathirika zaidi katika mji huo ni Buguruni kwa Mnyamani na eneo la
Jangwani katika Manispaa ya Ilala, ambako nyumba nyingi na barabara
zimeathirika. Sehemu nyingine za jiji la Dar es Salaam zimezingirwa na
maji kutokana na kuziba kwa mitaro na mifereji, ikiwa ni athari ya
utupaji taka ovyo na pia miundombinu duni. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali
ya Hewa nchini Tanzania (TMA), mvua kubwa zaidi zinatarajia kuendelea
kunyesha mpaka siku ya Jumatano. Kutokana na athari za mvua
zinazoendelea kunyesha, Mkuu wa Mko wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki
jana aliongoza kikosi cha uokoaji katika eneo la Buguruni kwa Mnyamani,
ambako nyumba 250 zilizingirwa na maji, jambo ambalo vikosi vya uokoaji
vililazimika kufanya kazi ya kuwanasua watu waliokuwa wamekwama katika
nyumba zao. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema kuwa, hadi kufikia
jana mvua hizo zilikuwa zimesababisha vifo vya watu watano, akiwemo mtu
mmoja aliyesombwa na maji, mwingine aliyeangukiwa na ukuta na watatu
ambao walinaswa na umeme baada ya nguzo ya umeme kuanguka Mbagala
Mzambarauni katika Manispaa ya Temeke.
IQRA FM RADIO
Monday, March 23
Mvua yasababisha vito vya watu 5 Dar es Salaam
Posted by mkachu | Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Related Posts:
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Sura ya Al Furqan, aya ya 41-44 (Darsa ya 628) Wasikilizaji wapenzi wa Darsa ya Qur'ani, Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: