Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Monday, March 23

Mvua yasababisha vito vya watu 5 Dar es Salaam

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Mvua yasababisha vito vya watu 5 Dar es Salaam  
 Hali tete inatawala katika jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania kutokana na mvua ya masika iliyonyesha kwa siku tatu na kusababisha vifo vya watu watano, huku nyumba nyingi zikiwa zimezingirwa na maji. Maeneo yaliyoathirika zaidi katika mji huo ni Buguruni kwa Mnyamani na eneo la Jangwani katika Manispaa ya Ilala, ambako nyumba nyingi na barabara zimeathirika. Sehemu nyingine za jiji la Dar es Salaam zimezingirwa na maji kutokana na kuziba kwa mitaro na mifereji, ikiwa ni athari ya utupaji taka ovyo na pia miundombinu duni. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA), mvua kubwa zaidi zinatarajia kuendelea kunyesha mpaka siku ya Jumatano. Kutokana na athari za mvua zinazoendelea kunyesha, Mkuu wa Mko wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki jana aliongoza kikosi cha uokoaji katika eneo la Buguruni kwa Mnyamani, ambako nyumba 250 zilizingirwa na maji, jambo ambalo vikosi vya uokoaji vililazimika kufanya kazi ya kuwanasua watu waliokuwa wamekwama katika nyumba zao. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema kuwa, hadi kufikia jana mvua hizo zilikuwa zimesababisha vifo vya watu watano, akiwemo mtu mmoja aliyesombwa na maji, mwingine aliyeangukiwa na ukuta na watatu ambao walinaswa na umeme baada ya nguzo ya umeme kuanguka Mbagala Mzambarauni katika Manispaa ya Temeke.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com