Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Thursday, September 25

“Maulamaa wajitahidi kuuarifisha Uislamu wa upendo”

Posted by mkachu  |  Tagged as:

“Maulamaa wajitahidi kuuarifisha Uislamu wa upendo”Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema jukumu la maulamaa na viongozi wa Kiislamu ni kufanya jitihada za kuimarisha umoja miongoni mwa Waislamu na kuutangaza Uislamu wa upendo hasa miongoni mwa vijana. Rouhani amesema hayo alipokutana na shakhshia na viongozi wa jamii ya Kiislamu ya Marekani mjini New York.

 Amebainisha kwamba adui anataka kukabiliana na Uislamu wa kisiasa kwa kuzusha mfarakano na hitilafu baina ya Waislamu na pia kuanzisha harakati za kigaidi kwa jina la kidini na jihadi. Rais Rouhani ameongeza kuwa, kuoneshwa vitendo vya kikatili na kishenzi katika mitandao ya kijamii kwa madai ya Uislamu, ni njama zenye lengo la kuudhalilisha Uislamu katika dunia iliyostaarabika ya leo. 

Katika upande mwingine, Rais wa Iran amekosoa vikwazo visivyo vya kibinadamu na vilivyo dhidi ya haki za binadamu vilivyowekwa na Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kutaka viondolewe. Pia amesema Tehran inashikamana na ahadi zake zote kwa mujibu wa makubaliano yaliyosainiwa kati ya Iran na kundi la 5+1 mwezi Novemba, kama njia ya kujenga uaminifu.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com